About us





Mmiliki wa blog hii ndugu Ahadi A.Mwakaniemba na  Mke wake Neema Ahadi wanakukaribisha sana katika blog hii ambayo itakuwezesha kupata maarifa mbalimbali. Tutajikita sana katika kutoa marrifa ya kilimo,ufugaji na biashara. Kupitia blog hii kampuni ikiwa ni shamba darasa la watu kujifunza maarifa ya namna ya kufuga kuku na nguruwe, kutengeneza bidhaa mbalimbali kama sabuni, mishumaa, Keki, Batiki, vikoi n.k,  kilimo cha mpunga, mahindi, Maharage, na bustani za mbogamboga na kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu biashara.
Kama kuna changamoto kubwa kipindi hiki ni changamoto ya ajira. Wale ambao wana sifa za kuajiriwa hawapati nafasi ya kuajiriwa. Pia wale ambao tayari wapo kwenye ajira, ajira zao haziwatoshelezi kwa kipato. Kipato wanachopata kwenye ajira hizo, hakiwezi kuwawezesha kufikia malengo yao haraka zaidi ya ajira hiyo kuwa chachu ya kuwapa nafasi ya kupanua wigo wa vitega uchumi vingine. Na kama inavyoeleweka, changamoto ya kipato cha ajira huchukua muda kuongezeka na hata kinapoongezeka kinaongezeka kidogo sana hivyo akili ya kufanikiwa kwa kutegemea mshahara utajikuta unaendelea kuwa maskini. Kwa mazingira hayo watu wasio na ajira na wale waajiriwa wanatakiwa kuangalia njia mbadala ya kuongeza kipato chao. Kupitia biashara na shughuli mbalimbali za ujasiriamali wanakuwa na uhakika wa kipato na kuelekea mafanikio.
Kupitia kitabu hiki utajifunza na kujua hatua mbalimbali ili kuanzisha biashara, ukianza na namna ya kupata wazo la biashara, uwezo mbalimbali anaotakiwa kuwa nao mjasiriamali katika kuanzisha biashara ikiwa ni pamoja na uwezo wa kutunza kumbukumbu, uwezo wa kusimamia fedha, uwezo wa kutafuta masoko na uwezo wa kuandika mchanganuo wa biashara ili kurahisisha utekelezaji wa uendeshaji wa biashara, na kujua nini ufanye ili biashara yako ikue na kuhimili ushindani unaoongezeka kila iitwapo leo katika biashara na jinsi ambavyo utaweza kuwa mshindani kupitia njia mbalimbali  ili uweze kufikia mafanikio makubwa kupitia ujasiriamali wako.
Mkurugenzi wa NEA GENUINE ENTERPRISES
Ndg AHADI MWAKANIEMBA
Contacts:
                  Gmail:    neagenuineideas@gmail.com                                                        
                You tube: NEA GENUINE TV

No comments:

Post a Comment

MAENDELEO

           JINSI YA KUANZISHA BIASHARA Uchumi wa Tanzania umekuwa ukizalisha ajira chache kila siku. Hii imekuwa ikifanya vijana wengi wa...