Friday, July 20, 2018

WITO WA UONGOZI


Wito Wa Mungu Kwetu Wa Kuongoza


“Natufanye mtu kwa mfano wetu….. akatawale”. (Mwanzo 1:26)


Kwa karne nyingi wakristo wamejadiliana juu ya suala la uongozi. Je, kuongoza ni kibiblia? Je, sisi hatukuitwa ili kuwa wafuasi badala ya viongozi? Je, hatukuitwa kuwa watumishi badala ya watawala? Je, tunaweza kuwa wakweli na kuamini kuwa uongozi ni wazo la kibiblia?


Tunapojifunza Biblia kwa karibu zaidi tunaona kuwa uongozi ni wazo la Mungu hasa. Si kwamba tu Mungu ni kiongozi wa juu kabisa lakini ametuita sisi pia kuongoza.


Tumezaliwa Kuongoza


            Fikiria hili. Maelezo ya mwanzo ya mwanadamu katika Biblia yanahusisha uongozi. Mungu alituumba kuongoza, kuwa na mamlaka na kutawala. Kulingana na Mwanzo 1:26 – 31, mimi na wewe tulizaliwa ili kuongoza. Soma kwa undani maandiko haya …


“Mungu akasema na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi”. (Mwanzo 1:26)


1. Kuumbwa kwa mfano wa Mungu kunamaanisha tuliumbwa ili ________.


Kulingana na mstari wa 26, tuliumbwa kwa mfano wa Mungu. Hii inamaana gani? Kidokezo kimoja kinapatikana katika kifungu kinachofuata “na wakatawale” Sehemu ya maana ya kuwa mfano wa Mungu ni kujua tuliumbwa kuongoza na kutawala.


2. Mungu aliwapa wanadamu _________ juu ya dunia yote


            Tunapaswa kujisikia vizuri juu ya nafasi mbili tulizo nazo. Nafasi ya kwanza ni kuwa chini ya mamlaka ya Mungu. Nafasi ya pili ni kuwa na mamlaka juu ya ulimwengu. Mungu ametupa sisi wito huu. Ni lazima tugundue ina maana gani kuongoza kama Mungu afanyavyo.
         3. Kama Mungu ametuambia tutawale, tunao________ wa kufanya hivyo.


            Mungu kamwe hatuamuru kufanya kitu bila kutupa uwezo wa kufanya kitu hicho. Wewe na mimi tuna uwezo wa kuongoza kwa sababu Mungu alituumba na kutuamuru kufanya hivyo. Kwa kuzingatia vipawa vyako na haiba yako una uwezo wa kuongoza katika maeneo fulani.


            Kuwa Chumvi Na Nuru

            Katika agano jipya, Mungu anathibitisha wito huu wa kuwashawishi wengine. Angalia Mathayo 5:13-16:  “Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima, wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani. Vivyo hiyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.


Chumvi huathiri chakula tunachokula. Nuru huathiri nyumba tunazoishi. Yesu anatuita kukumbatia wito wetu wa kushawishi na kuangaza popote tuendako. Mtume Paulo alitilia maanani wito huu pale aliposema:


“Basi tukiijua hofu ya Bwana, twawavuta wanadamu…” (2 Wakorintho 5:11)


Ruhusa ya kimungu ya kuongoza


Wengi wetu hujisikia kama Musa alivyojisikia alipokabiliana na Mungu katika kichaka kilichowaka moto katika Kutoka 3 – 4. Alijisikia mpungufu na asiye na maandalizi ya kuongoza. Lakini hicho ndicho Mungu alichomuitia kufanya. Viongozi wengi wakuu wa Biblia waliogopa na kuukimbia wito huo. Ilibidi Mungu awape ruhusa ya kufanya hivyo.


Wengi wetu tunaweza kutoa sababu zinazotufanya kutokuongoza vizuri, kama Musa alivyofanya. Mungu alipomuita, mara moja, alikuwa na sababu tano za kushindwa kuongoza. Tambua jinsi Mungu alivyojibu kuhusu sababu hizo.


Udhuru wa kwanza: Mimi ni nani? (Kutoka 3:11)

Musa alisumbuka juu ya utambulisho wake. Hakujisikia kama alikuwa anastahili. Alifikiri Mungu alichagua kiongozi asiye sahihi. Mwitikio wa Mungu si kitu wewe u nani. Nimekuita. Niko pamoja na wewe.


Udhuru wa pili: Wewe ni nani? (Kutoka 3:13)

Musa alisumbuka na uhusiano wa karibu. Hakumjua Mungu kiasi cha kutosha kumuelezea kwa watu. Uhusiano wake na Mungu ulikuwa dhaifu. Mwitikio wa Mungu: Mimi Niko ambaye Niko. Mimi ni kila kitu unachohitaji.


Udhuru wa tatu: Itakuwaje wasipokubali kusikiliza (Kutoka 4:1)

Musa alisumbuka na woga. Aliogopa juu ya mwitikio wa watu juu yake. Mwitikio wa Mungu katika utimilifu wangu, watasikiliza. Nitumaini mimi.


Udhuru wa nne: Sijawahi kuwa mnenaji mzuri (Kutoka 4:10)

Musa alisumbuka na upungufu. Nani angemfuata wakati hakuweza kuzungumza vizuri? Mwitikio wa Mungu: Fikiri nani aliufanya mdomo wako? Mimi ndiye chanzo cha vipawa vyako.


Udhuru wa tano: Najua unaweza kupata mwingine (Kutoka 4:13)

Musa alisumbuka na kujidharau. Alijilinganisha na watu wengine wenye uwezo zaidi yake na akajiona hafai. Mwitikio wa Mungu. Sawa, utakwenda na Haruni… lakini bado nakuita wewe.


SWALI: Una udhuru gani kwa kutokuongoza vizuri? Unaamini mwitikio wa Mungu waweza kuwaje?





IJUE NAFASI AMBAYO MUNGU AMEKUPA





No comments:

Post a Comment

MAENDELEO

           JINSI YA KUANZISHA BIASHARA Uchumi wa Tanzania umekuwa ukizalisha ajira chache kila siku. Hii imekuwa ikifanya vijana wengi wa...