Monday, July 23, 2018

WAKATI NA MAJIRA

ISHI KATIKA WAKATI NA MAJIRA

Mungu alipo muumba mwanadmu alikuwa na mpango mzuri haijarishi kabila lako, kimo chako, utajiri wako, bara lako au nchi uliyozaliwa. Lakini pamoja na hayo mwanadamu huyu huyu akamkosea Mungu kupitia udanganyifu wa Ibilisi Shetani na kuondokewa na utukufu.
Hivyo Mungu akaandaa mpango wa kurudisha uhusiano uliokuwa umepotea kupitia jina la mwanaye wa peke Yesu Kristo ili kila amwaminiye sipotee bali awe na uzima wa milele. 
Yohana 3:16

Si kwamba tulistahili kufanyiwa hivyo ni neema tu ya Mungu baada ya kuona adha na mateso tunayopata, kwa maana nyingine ni kwamba tusingeweza kulipa gharama lakini Mungu kwa kuwa ni mwingi wa rehema akamua kumtoa mwanaye ili tuhuishwe kwa damu yake, kwahiyo tumeokolewa kwa neema, kwanini nasema kwa neema kwasababu Neema ni stahili ambayo mtu hupata/kupewa hata kama mtu huyo hakustahili.
Waefeso 2:1-5


Sasa watu wengi wamekuwa wakilaumu wanapopitia changamoto, Sulemani ameeleza kuwa kila jambo kuna majira yake na wakati wakila kusudi chini ya mbingu na ameeleza nyakati nyingi sana.
Mhubiri 3:1-12

 Lakini baadaye alipozieleza nyakati hizo na majira tena akasema "Siku ya kufanikiwa ufurahi, na siku ya mabaya ufikiri. Mungu ameifanya ...
Mhubiri 7:14.
Mungu ndiye anayejua changamoto, majaribu na wakati mgumu unaopitia, hivyo mtumaini yeye ili ufike mwisho wako salama na kesho yako iko mikononi mwake, Ayubu aliona amelemewa akatambua kwamba hakuja na kitu duniani atarudi bila kitu akasema " Lakini yeye aijua njia niendeayo akisha kunijaribu nitatoka kama dhahabu. "
Ayubu 23:10
 Mungu akubariki jipe moyo mkuu kwa hilo linalokusumbua utashinda

No comments:

Post a Comment

MAENDELEO

           JINSI YA KUANZISHA BIASHARA Uchumi wa Tanzania umekuwa ukizalisha ajira chache kila siku. Hii imekuwa ikifanya vijana wengi wa...